KITENDO cha kutekwa na kupigwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka, kumeibua hisia kali kwa madaktari waliopo katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, huku wakisema kuwa Serikali haiwezi kukwepa kuhusiana na kitendo hicho.
Wakizungumza na Mwananchi, madaktari waliogoma hospitalini hapo huku wakikataa kabisa kuandikwa majina yao walisema, watanzania wanatakiwa kutambua wazi kwamba Serikali imetangaza vita na madaktari hao na kwamba wameitaka Serikali kutolea ufafanuzi yakinifu kuhusiana na kupigwa kwa kiongozi huo.
Walisema kitendo cha kutekwa kwa Dk Ulimboka, kamwe hawapo tayari kurudi kazini licha ya kuwa baadhi yao walikuwa tayari kurejea kazini lakini kutokana na hilo hawawezi kumsaliti Ulimboka kwa kitendo alichofanyiwa, na kudai kuwa ndio kwanza mgomo huo umeanza rasmi sasa uliopita haukuwa mgomo.
“Kamwe sisi hatupo tayari kurudi kazini tena, kwanza ndio mgomo umeanza rasmi na kutokana na hali hii watanzania watambue wazi kwamba serikali imechoka, tumetoka vijijini tutarudi kulima, lakini hatutamsaliti Ulimboka” alisema mmoja wa madaktari hao huku akitokwa machozi.
Daktari huyo ambaye yupo katika mafunzo ya vitendo alisema kuwa kumpoteza Dk Ulimboka siyo mwisho wa kudai haki kwa kuwa ulimboka ni kiongozi tu na suala la kudai maslahi yao yapo mikononi mwao hivyo wataendelea na harakati zao hadi kitakapo eleweka.
“Kumwagika kwa damu ya Ulimboka kumetengeneza akina Ulimboka wengi na damu yake italipwa na sisi kwa kutomsaliti kwa namna yoyote ile na hiyo damu ya mpigaji mwenzetu ndio kwanza imefumbua makucha yetu kuanzia sasa” alisema daktari huyo.
Hata hivyo, Daktari bingwa ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe alisema, kitendo cha kutekwa kwa Dk Ulimboka hata wao ambao hawakuwapo katika mgomo huo sasa, wanaingia kwenye mgomo huo rasmi kwa kile alichodai kuwa ulimboka ni daktari kama wao.
Thursday, June 28, 2012
Wednesday, June 27, 2012
Serikali inawajibika kutueleza: Dkt. Ulimboka kutekwa, kupigwa na kuumizwa - Zitto Kabwe
Ujumbe amenitumia Daktari yupo pale MOI
‘Kaka Zitto,hali ya Dr.Ulimboka yuko unconscious,multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya,yuko icu wanamstabilise kwanza kwasababu hapumui vizuri,the situation here is really bad, I agree with you this is outright outrageous’
Nimechukizwa sana na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dr Ulimboka, Kiongozi wa Madaktari Nchini. Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika Taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko. Nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dokta Ulimboka na kujulishwa kwamba majeruhi huyu wa vitendo vya hovyo kabisa kutokea hapa nchini alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa MagwePande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.
Serikali kama mlinzi wa usalama kwa raia inaWAJIBU kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake. Serikali INAWAJIBIKA kueleza katika nyakati kama hizi ambapo kuna mgogoro kati yake na madaktari imekuwa wapi kuhakikisha usalama wa viongozi wa madaktari ili kuepusha watu wanaoitwa ‘agente provocateure‘ kuweza kuhatarisha hali ya amani ya nchi na hata kupelekea kuweka hali ya vitisho kwa madaktari wetu.
Serikali INAWAJIBIKA kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.
Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya wa CHADEMA kufuatilia suala hili kwa kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote na ukweli mtupu unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake. ‘An injury to one, injuries to all’
Naomba madaktari wamwangalie kwa karibu daktari mwenzao ili aweze kupata nafuu. Ulinzi uimarishwe ili kuhakikisha usalama wake.
via ZittoKabwe.com
Tuesday, June 26, 2012
54 wanusurika ajali ya Ngorika Arusha
ABIRIA zaidi ya 54 wamenusurika kifo baada ya basi la Ngorika
walilokuwa wakisafiria kutoka Arusha kwenda jijini Dar es Salaam kupinduka
eneo la Kwa Mrefu majira ya saa 12:10 jana asubuhi,nje kidogo ya mji wa Arusha
walilokuwa wakisafiria kutoka Arusha kwenda jijini Dar es Salaam kupinduka
eneo la Kwa Mrefu majira ya saa 12:10 jana asubuhi,nje kidogo ya mji wa Arusha
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Arusha, Liberatus Sabas, alisema katika ajali hiyo, abiria mmoja
Hashim Mohammed (31), mkazi wa Mwanza
alijeruhiwa na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Arusha, Liberatus Sabas, alisema katika ajali hiyo, abiria mmoja
Hashim Mohammed (31), mkazi wa Mwanza
alijeruhiwa na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Kamanda Sabas alisema kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa chanzo
cha ajali hiyo kilikuwa ni utelezi uliotokana na mvua iliyonyesha na
dereva kushindwa kushika breki,na alipofanikiwa kushika breki gari
lilianguka huku magurudumu yakiwa juu.
cha ajali hiyo kilikuwa ni utelezi uliotokana na mvua iliyonyesha na
dereva kushindwa kushika breki,na alipofanikiwa kushika breki gari
lilianguka huku magurudumu yakiwa juu.
Alisema basi hilo lenye namba za usajili T 580 BBL, aina ya
Utong,lilikuwa likienedshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Nuru
Mdee (45) mkazi wa Dar es Salaam, anashikiliwa na polisi.
Utong,lilikuwa likienedshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Nuru
Mdee (45) mkazi wa Dar es Salaam, anashikiliwa na polisi.
Alifafanua kuwa baada ya mahojiano na upelelezi kukamilika,devera huyo
anaweza kufikishwa katika vyombo vya sheria na kuwahimiza madereva
kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani.
anaweza kufikishwa katika vyombo vya sheria na kuwahimiza madereva
kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani.
Short URL: http://www.thehabari.com
Waliochaguliwa kufanya usaili Jeshi la Polisi hadharani
Na Mwandishi Wetu, Musoma
JESHI la Polisi Mkoa wa Mara limetoa majina ya vijana ambao wamechaguliwa kwa ajili ya kufanya usaili wa kujiunga na jeshi hilo ambapo kanda ya ziwa utafanyika Julai 2 hadi 4 mwaka huu katika ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Absalom Mwakyoma alisema kuwa majina hayo yatabandikwa kwenye mbao za matangazo zilizopo katika ofisi za Mkoa na wilaya zote.
“Mwaka huu tumeamua kuchukua vijana watakaojiunga na jeshi letu kutoka mashuleni ambao wamemaliza kidato cha nne mwaka jana na cha sita mwaka huu hivyo tunawaamba vijana wote waende wasome na wajue kama jina lake lipo katika orodha yetu,”
“Hii tumerahisisha ili kupunguza msongamano wa vijana kufika katika ofisi zetu na kuulizia ajira hizo na kama unatumia mtandao tafuta katika mtandao wetu wa www.policeforce.go.tz na utaona jina lako na vituo vya usaili,”alisema.
Alisema kuwa vijana ambao wataona majina yao waende katika kituo cha usaili katika kanda mbalimbali kama zitavyoonesha katika matangazo yao wakiwa na vyeti halisi vya masoma yake na cheti cha kuzaliwa.
“Tunasisitiza kwa watahiniwa kufika katika vituo hivyo na vyeti vyao pia tunawakumbusha kuwa hati ya kiapo ya mahakamani haitakubaliwa na awe na barua ya wadhamini wawili wanaomfahamu vizuri zinazoelezea mahusiano baina yao na muombaji na namba za simu na anuani halisi ambazo zinatumika,”alisema Kamanda Mwakyoma.
Alisema kuwa kila kijana ambaye ataona jina lake atajigharamia gharama zote za usafiri, chakula na malazi muda wote wa usaili pamoja na kalamu za wino kwa ajili ya kuandikia.
Kamanda Mwakyoma alisema kuwa mtahiniwa anaruhusiwa kufanya usaili katika kanda yoyote kulingana na tarehe husika kuepusha usumbufu wa kusafiri safari ya mbali.
Jeshi hilo la Polisi limeamua kutumia mfumo huo ambao ulikuwa unatumika miaka ya nyuma walikuwa wanatoa moja kwa moja mashuleni ili kuepusha upendeleo na malalamiko kwa wanyonge.
http://www.thehabari.com
Taarifa ya Mahakama Kuu Tanzania kusitisha mgomo wa madaktari
KUFUATIA Tangazo la Chama cha Madaktari nchini (MAT) la kuanza mgomo siku ya Jumamosi tarehe 23 Juni, 2012, Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha kazi, Dar es Salaam imetoa amri ya kusitisha mgomo huo mpaka hapo pande zote mbili yaani Serikali na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
• Amri hiyo ya Mahakama imetolewa kufuatia maombi namba 73 ya 2012 yaliyowasilishwa chini ya hati ya dharura na Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT). Sababu za msingi amabazo zimepelekea Mahakama kuu kutoa amri hiyo upande mmoja ni pamoja na;
• Iwapo mgomo huo utatokea utakuwa na kuwa amri hii isipotolewa madhara yake ni makubwa isiyoweza kufidiwa kwa namna yoyote ile kama vile kupoteza maisha n.k
• Wajibu maombi,ambao ni MAT, inaundwa na Madaktari ambao wapo katika Sekta ambayo inatoa huduma mahsusi (essential service sector), Aidha Chama cha Madaktari Tanzania kimetangaza mgomo bila kufuatia taratibu zilizoanishwa katika Kifungu cha 76(1 na 2) cha Sheria ya Kazi (Employment and Labour Relations Act No 6 ya 2004.
Masharti hayo ni
• Kuzuia wafanyakazi walio katika Sekta Muhimu kugoma na kama wakigoma,
• Kuwepona makubalianao ya pamoja ya kutoa huduma za msingi wakati mgomo ukiendelea.
Kwa misingi hii, Mahakama Kuu ya Tanzania, kwa Chama cha Madktari Nchini na wanachama wake kusitisha na kutoshiriki katika mgonmo huo.
Masharti hayo ni
• Kuzuia wafanyakazi walio katika Sekta Muhimu kugoma na kama wakigoma,
• Kuwepona makubalianao ya pamoja ya kutoa huduma za msingi wakati mgomo ukiendelea.
Kwa misingi hii, Mahakama Kuu ya Tanzania, kwa Chama cha Madktari Nchini na wanachama wake kusitisha na kutoshiriki katika mgonmo huo.
Monday, June 25, 2012
"Chanzo ni udhaifu wa Naibu Spika Ndugai ", nitamkatia rufaa kupitia Kamati - Mnyika
MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika amesema anakusudia kukata rufaa kwa Kamati ya Bunge ya Kanuni dhidi ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kutokana na uamuzi wa kumtoa bungeni wiki iliyopita.
Wiki iliyopita Mnyika alitolewa bungeni baada ya kukataa kufuta kauli yake kuwa ‘Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu’.
Jana, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mnyika alisema anakusudia kukata rufaa dhidi ya Ndugai, ili kuwe na mjadala mpana wa kibunge utakaoweka kumbukumbu sahihi.
Alisema uamuzi huo wa kukata rufaa kwa Kamati ya Kanuni za Bunge, unalenga kupata haki.
Mnyika alisema kutamka kuhusu udhaifu wa Rais, si kumtukana wala siyo kutumia jina lake kwa dhihaka.
“Pamekuwapo na propaganda za kudai kuwa kauli hiyo ni matusi, chanzo ni udhaifu wa Naibu Spika Ndugai, kwa kunihukumu kwa kutumia kanuni tofauti na tuhuma iliyotolewa,” alisema.
Alifafanua kwamba, “Naheshimu taasisi ya urais na umri, naamini pia katika matumizi ya lugha za kidiplomasia, hata hivyo, niliamua kuusema ukweli kwa lugha ya moja kwa moja ili ujumbe ufike kwa mamlaka zote.”
Alisema hata viongozi wa dini na taasisi mbalimbali, wamekuwa wakisema hadharani kuhusu udhaifu huo wa rais.
Kuhusu Bajeti, Mnyika alisema wabunge wamekuwa na udhaifu kutokana na Katiba kuweka nguvu kubwa kwa Rais, kwamba wasipopitisha Bajeti anaweza kulivunja Bunge.
“ Woga huo wa Rais kulivunja Bunge ndiyo maana wamekuwa wakipitisha Bajeti kwa kauli za `ndiyo’ kwa asilimia 100, hata kama kuna maeneo ambayo wanayapinga,” alisema Mnyika katika taarifa yake hiyo.
Mbali na kukata rufaa, aliongeza, “Bunge litakapokuwa likijadili utekelezaji wa bajeti katika Ofisi ya Rais 2012/13, nitaeleza hatua ambazo Rais anapaswa kuchukua kufanikisha ahadi alizozitoa kwa Watanzania.”
Alisema anaamini, Rais Kikwete anayo fursa ya kurekebisha, ili kuongeza nguvu zake katika kupanua wigo wa mapato na hatimaye kuongeza kiwango cha fedha za maendeleo.
via jamiiforums.com na Gazeti la mwananchi
Wiki iliyopita Mnyika alitolewa bungeni baada ya kukataa kufuta kauli yake kuwa ‘Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu’.
Jana, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mnyika alisema anakusudia kukata rufaa dhidi ya Ndugai, ili kuwe na mjadala mpana wa kibunge utakaoweka kumbukumbu sahihi.
Alisema uamuzi huo wa kukata rufaa kwa Kamati ya Kanuni za Bunge, unalenga kupata haki.
Mnyika alisema kutamka kuhusu udhaifu wa Rais, si kumtukana wala siyo kutumia jina lake kwa dhihaka.
“Pamekuwapo na propaganda za kudai kuwa kauli hiyo ni matusi, chanzo ni udhaifu wa Naibu Spika Ndugai, kwa kunihukumu kwa kutumia kanuni tofauti na tuhuma iliyotolewa,” alisema.
Alifafanua kwamba, “Naheshimu taasisi ya urais na umri, naamini pia katika matumizi ya lugha za kidiplomasia, hata hivyo, niliamua kuusema ukweli kwa lugha ya moja kwa moja ili ujumbe ufike kwa mamlaka zote.”
Alisema hata viongozi wa dini na taasisi mbalimbali, wamekuwa wakisema hadharani kuhusu udhaifu huo wa rais.
Kuhusu Bajeti, Mnyika alisema wabunge wamekuwa na udhaifu kutokana na Katiba kuweka nguvu kubwa kwa Rais, kwamba wasipopitisha Bajeti anaweza kulivunja Bunge.
“ Woga huo wa Rais kulivunja Bunge ndiyo maana wamekuwa wakipitisha Bajeti kwa kauli za `ndiyo’ kwa asilimia 100, hata kama kuna maeneo ambayo wanayapinga,” alisema Mnyika katika taarifa yake hiyo.
Mbali na kukata rufaa, aliongeza, “Bunge litakapokuwa likijadili utekelezaji wa bajeti katika Ofisi ya Rais 2012/13, nitaeleza hatua ambazo Rais anapaswa kuchukua kufanikisha ahadi alizozitoa kwa Watanzania.”
Alisema anaamini, Rais Kikwete anayo fursa ya kurekebisha, ili kuongeza nguvu zake katika kupanua wigo wa mapato na hatimaye kuongeza kiwango cha fedha za maendeleo.
via jamiiforums.com na Gazeti la mwananchi
Maongezi na Daktari wa Muhimbili - UKWELI KUHUSU MGOMO WA MADAKTARI
MADAI
MAKUBALIANO
HALI ILIVYO SASA
- HOSPITALINI: hakuna huduma za afya (matibabu, upimaji wala upasuaji), YAANI NI KWELI TUMEGOMA
- VYOMBO VYA HABARI: Kuna upotoshwaji mkubwa wa taarifa kwa umma.
- MTAANI: Hofu na mashaka kwa wananchi kutokana na kutoelewa matamko yanayopingana kati ya Serikali na Tamko la madaktari
MTAZAMO
HEBU ANGALIA KATIKA MAKUBALIANO NI LIPI LIMETEKELEZWA HADI SASA?? THEN SERIKALI INAONGEZA MISHAHARA YA WABUNGE, HIVI KARIBUNI UTASIKIA SABASABA!!!
- Jumla ya madaktari wote ni chini ya 15,000 (na hapa namaanisha General practitioners and Specialists). Kwa uchache au wingi wetu tumekwisha kuona madhara ya migomo miwili iliyokwishatokea.Nashangwazwa na kuona baadhi ya watu wanaosema madaktari hatuna utu wala huruma na tunaweka maslahi yetu mbele, hivi mnajua kuwa katika nchi za East and Central Africa, Tanzania ndiyo yenye kulipa mishahara midogo kwa watu wa sekta ya Afya?? Rwanda juzi juzi (1994) walikuwa na vita lakini daktari analipwa 1500USD, au mnadhani hatujui kuna nchi za jirani na mbali tunaweza kwenda kama wenzetu (Mf. Rwanda, Botswana, Zambia, Lesotho, Egypt, SA, nk) ??? mnadhani kubaki kwetu Tanzania tuteseke kwa kauli eti “UDAKTARI NI WITO?”, “WATANZANIA -WATOTO, KINA MAMA, NA WAZEE WATAKUFA IWAPO TUKIGOMA”, “OOOH?? HATUTAKIWI KUGOMA”…tumeonyesha uzalendo wetu kwa kubaki hapa hapa na mazingira yetu magumu, lakini sasa IMEFIKA MWISHO.
Pediatrics(wodi ya watoto):Hakuna vifaa vya kuongezea maji/damu mwilini(cannula), hakuna mitungi ya gesi, OBGYN(wodi ya kina mama);hakuna pamba, mipira ya mikojo(urine bags), MOI, Mwaisela hakuna vitanda, Operating Theatre,OT; Hakuna gloves ,mask, kofia za kutosha, Huduma ya mionzi ya CT SCAN ni mwezi wa saba haifanyi kazi(huku mmiliki akiwa anaidai Wizara ya Afya mil.800/=Tsh)na haitakuwepo hadi atakapolipwa.
Kwa madai hayo, si lazima serikali itekeleze all at once, lakini Mshahara unazungumzika, wale mnaofanya interview, huwa hamuulizwi ni kiasi gani unategemea kuanza nacho na waajiri wenu? Doesn’t this make salary being negotiable?? Then kwanini isiwe kwetu?
Hivi ulishawahi kusikia MASS RESIGNATION????? It takes ATLEAST 12yrs kumpata huyo specialist after elimu ya sekondari, Halafu nasikia mnasema eti tufukuzwe kazi?Then what??? Kwa wale wenye mtazamo mfupi mnadhani Serikali inaweza ku-import madaktari toka nje.
Kwa mfano:
Then NASIKIA MTATUPELEKA MAHAKAMANI.
Utawakamata madaktari wote nchini?? Kumbuka huu mgomo hauna kikomo na hauna kiongozi!!!..hypothetically speaking ukitupeleka, tutawatibu tukiwa huko gerezani?? Waliobaki mnadhani watarudi makazini?tukirudi mnadhani tutafanya kazi? Tukifanya kazi unadhani itakuwa katika kiwango kinachotakiwa? With demoralization unategemea tutaponyesha ndugu zetu kweli, au mortality kuwa juu??? Then kwa wanafunzi walio vyuo vya tiba kama MUHAS, WBUCHS, KCMC, UDOM, HKMU, IMTU..watafanya kazi hapa nchini kwa hali hii, ama Brain drain ndiyo itazidi!!
SIASA
Wananchi walishazoea kudanganywa, na hii imezoeleka na viongozi Fulani kushindwa kufanya wajibu wao kusingizia wanasiasa kadhaa..Hapa HAKUNA siasa ila mkiileta tutawaachia tu kwani huko hatupawezi ila viongozi mjue hakuna tena rufaa ya kwenda nje (mf. INDIA) MUHIMBILI
Hivi wananchi mnajua viongozi wanalipwa kiasi gani wanapoenda nje kutibiwa na familia???
Eti kwa sababu sekta nyingine hawawezi kugoma, ndio na sisi tusigome? Eti kwa sababu askari anayetumia SMG na kupambana na jambazi anayetumia AK47, eti kwa sababu mishahara ya walimu inacheleweshwa, ndio tusigome??? Nani kasema??
HITIMISHO
HAPA KAZINI HATURUDI…HII IELEWEKE VIZURI…HATURUDI….MGOJA NIIWEKE VIZURI HATURUDI, ACHA MEDIA IENDELEE KUDANGANYA, LAKINI UKWELI TUNAUJUA, MWISHONI MTARUDI TU, NA THIS TIME SI TENA YA KUTUMIA BUSARA ZETU KUWASTAHI VIONGOZI NA KISHA KWENDA PALE KUONGEA NA ‘WAZEE WA DSM”
“Doctors we might be slow walkers, but we never walk back” Solidarity Forever!
from wavuti.com
- Kuboresha Huduma za afya hospitalini kwa vifaa vya upimiaji, madawa.
- Kuboresha Mazingira Ya kazi (ukarabati wa majengo, uongezaji wa vitanda)
- Posho ya muda wa ziada wa kazi (call allowance) 5% kama ilivyo kisheria kwa kada yoyote.
- Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu 40% (MEANING anayefanya kazi SAME, TANDAHIMBA, NYAMPULUKANO nk ni tofauti na akaaye MJINI)
- Posho ya makazi 40% au nyumba kama ilivyo kisheria(since DOCTOR IS ENTITLED KUPATA, HII NI KATIKA SHERIA YAO WENYEWE)
- Bima ya Afya (Green Card) kwa wafanyakazi wote wa sekta ya Afya.
- Kuwaondoa viongozi wa juu wa W/Afya kutokana na ubadhirifu.
- Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi 30% au Chanjo(Homa ya ini-hepatitis, HIV/AIDS, TB)
MAKUBALIANO
- Kuondolewa kwa viongozi na watendaji wa juu wa Wizara ya Afya
- Kupewa nusu ya ombi la call allowance hadi pale baada ya mazungumzo(ktk kipindi cha mpito)
- Kamati kujadili na kuona kiasi gani mshahara na posho zitaongezwa kwa kutengeneza(developing a formula)
- Serikali kuongeza bajeti ya W/Afya ili kuongeza vifaa, na madawa.
HALI ILIVYO SASA
- HOSPITALINI: hakuna huduma za afya (matibabu, upimaji wala upasuaji), YAANI NI KWELI TUMEGOMA
- VYOMBO VYA HABARI: Kuna upotoshwaji mkubwa wa taarifa kwa umma.
- MTAANI: Hofu na mashaka kwa wananchi kutokana na kutoelewa matamko yanayopingana kati ya Serikali na Tamko la madaktari
MTAZAMO
HEBU ANGALIA KATIKA MAKUBALIANO NI LIPI LIMETEKELEZWA HADI SASA?? THEN SERIKALI INAONGEZA MISHAHARA YA WABUNGE, HIVI KARIBUNI UTASIKIA SABASABA!!!
- Jumla ya madaktari wote ni chini ya 15,000 (na hapa namaanisha General practitioners and Specialists). Kwa uchache au wingi wetu tumekwisha kuona madhara ya migomo miwili iliyokwishatokea.Nashangwazwa na kuona baadhi ya watu wanaosema madaktari hatuna utu wala huruma na tunaweka maslahi yetu mbele, hivi mnajua kuwa katika nchi za East and Central Africa, Tanzania ndiyo yenye kulipa mishahara midogo kwa watu wa sekta ya Afya?? Rwanda juzi juzi (1994) walikuwa na vita lakini daktari analipwa 1500USD, au mnadhani hatujui kuna nchi za jirani na mbali tunaweza kwenda kama wenzetu (Mf. Rwanda, Botswana, Zambia, Lesotho, Egypt, SA, nk) ??? mnadhani kubaki kwetu Tanzania tuteseke kwa kauli eti “UDAKTARI NI WITO?”, “WATANZANIA -WATOTO, KINA MAMA, NA WAZEE WATAKUFA IWAPO TUKIGOMA”, “OOOH?? HATUTAKIWI KUGOMA”…tumeonyesha uzalendo wetu kwa kubaki hapa hapa na mazingira yetu magumu, lakini sasa IMEFIKA MWISHO.
Pediatrics(wodi ya watoto):Hakuna vifaa vya kuongezea maji/damu mwilini(cannula), hakuna mitungi ya gesi, OBGYN(wodi ya kina mama);hakuna pamba, mipira ya mikojo(urine bags), MOI, Mwaisela hakuna vitanda, Operating Theatre,OT; Hakuna gloves ,mask, kofia za kutosha, Huduma ya mionzi ya CT SCAN ni mwezi wa saba haifanyi kazi(huku mmiliki akiwa anaidai Wizara ya Afya mil.800/=Tsh)na haitakuwepo hadi atakapolipwa.
Kwa madai hayo, si lazima serikali itekeleze all at once, lakini Mshahara unazungumzika, wale mnaofanya interview, huwa hamuulizwi ni kiasi gani unategemea kuanza nacho na waajiri wenu? Doesn’t this make salary being negotiable?? Then kwanini isiwe kwetu?
Hivi ulishawahi kusikia MASS RESIGNATION????? It takes ATLEAST 12yrs kumpata huyo specialist after elimu ya sekondari, Halafu nasikia mnasema eti tufukuzwe kazi?Then what??? Kwa wale wenye mtazamo mfupi mnadhani Serikali inaweza ku-import madaktari toka nje.
Kwa mfano:
- Ni nchi gani itakuazima madaktari?? Kwa mshahara upi na vifaa gani? CUBA-3000USD, RWANDA-1500USD!!!
- Hypothetically speaking, wakikusaidia madaktari, watakupatia wangapi??
- Apartment na transport allowances utawapa kiasi gani?
- Hivi bibi aliye Tandahimba, asiyejua Kiswahili vizuri ataweza kuongea kiingereza na hao doctors??ama utahitaji wakalimani(translators), if so wangapi??? Utawalipa??
- Then hao madaktari watakaa hapa milele??
Then NASIKIA MTATUPELEKA MAHAKAMANI.
Utawakamata madaktari wote nchini?? Kumbuka huu mgomo hauna kikomo na hauna kiongozi!!!..hypothetically speaking ukitupeleka, tutawatibu tukiwa huko gerezani?? Waliobaki mnadhani watarudi makazini?tukirudi mnadhani tutafanya kazi? Tukifanya kazi unadhani itakuwa katika kiwango kinachotakiwa? With demoralization unategemea tutaponyesha ndugu zetu kweli, au mortality kuwa juu??? Then kwa wanafunzi walio vyuo vya tiba kama MUHAS, WBUCHS, KCMC, UDOM, HKMU, IMTU..watafanya kazi hapa nchini kwa hali hii, ama Brain drain ndiyo itazidi!!
SIASA
Wananchi walishazoea kudanganywa, na hii imezoeleka na viongozi Fulani kushindwa kufanya wajibu wao kusingizia wanasiasa kadhaa..Hapa HAKUNA siasa ila mkiileta tutawaachia tu kwani huko hatupawezi ila viongozi mjue hakuna tena rufaa ya kwenda nje (mf. INDIA) MUHIMBILI
Hivi wananchi mnajua viongozi wanalipwa kiasi gani wanapoenda nje kutibiwa na familia???
Eti kwa sababu sekta nyingine hawawezi kugoma, ndio na sisi tusigome? Eti kwa sababu askari anayetumia SMG na kupambana na jambazi anayetumia AK47, eti kwa sababu mishahara ya walimu inacheleweshwa, ndio tusigome??? Nani kasema??
HITIMISHO
HAPA KAZINI HATURUDI…HII IELEWEKE VIZURI…HATURUDI….MGOJA NIIWEKE VIZURI HATURUDI, ACHA MEDIA IENDELEE KUDANGANYA, LAKINI UKWELI TUNAUJUA, MWISHONI MTARUDI TU, NA THIS TIME SI TENA YA KUTUMIA BUSARA ZETU KUWASTAHI VIONGOZI NA KISHA KWENDA PALE KUONGEA NA ‘WAZEE WA DSM”
“Doctors we might be slow walkers, but we never walk back” Solidarity Forever!
from wavuti.com
Mohammed Mursi atangazwa mshindi wa urais Misri
MURSI ameshinda kura kwa asilimia 51.7 akimshinda mpinzani wake wa karibu Ahmed Shafik kwa mujibu wa taarifa ya Tume ya Uchaguzi wa juu wa Rais. Mkuu wa jopo la Majaji, Farouq Sultan, amesema kua wamezingatia malalamiko 466 kutoka kwa wagombea, ingawa matokeo ya uchaguzi hayatobalika.
Tangazo hilo lilifuatiwa na shangwe na vigelegele katikakati ya medani ya Tahrir mjini Cairo ambako wafuasi wengi wa Mursi walikua wamekuanyika.
Wafuasi hao wamekaa kwenye medani hio kwa siku kadhaa wakionyesha msimamo wao wa kuchukia sheria kadhaa zilizotangazwa na Baraza la juu la utawala wa majeshi ambayo wanadai zimeundwa ili kupunguza mamlaka ya Rais na kuelekeza uwezo mkubwa kwa majeshi. Wafuasi wa Shafiq nao waliweka kambi yao katika eneo la kaskazini mwa mji ambako kuna makao makuu ya Tume ya uchaguzi huko Nasser City.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi Jaji Sultan alianza kwa kunena kua tangazo la matokeo ya uchaguzi yalikua yamezongwa na shinikizo pamoja na hali ya wasiwasi. Tume ya uchaguzi ilizingatia sheria ilipochunguza visanduku vya kupigia kura, na Jaji.
Sultan alisema hakuna kilicho juu ya sheria. Jaji huyo akaongezea kukanusha madai mawili nyeti kuhusu njama za kuibia uchaguzi, kwamba baadhi ya karatasi za kupigia kura ziliwekwa ndani ya visanduku tayari zikiwa na majina ya mgombea wanayemtaka ashinde.
Hatimaye Jaji Sultan akamtangaza mshindi kua ni Mursi ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha Muslim Brotherhood cha Freedom and Justice, Mursi.
Baada ya dakika kadhaa akitangaza marekebisho kuhusu matokeo madomadogo ya kura ndipo akamtangaza Mursi kua mshindi kwa kuzoa kura 13,230,131, na Shafiq akiweza kuzoa 12,347,380, sawa na asilimia 48.27.
Marehemu Willy Edward azikwa Morotonga Mugumu
Na Mwandishi Wetu, Morotonga Mugumu
MWILI wa aliyekuwa mwanahabari na Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Willy Edward Ogunde amezikwa jana jioni (majira ya saa tisa) kijijini kwao Morotonga Mugumu, wilayani Serengeti katika Mkoa wa Mara.
Marehemu Edward Ogunde amezikwa kijijini hapa eneo la makaburi ya familia yao Morotonga baada ya ibada ya maziko iliyoanza majira ya saa tano asubuhi, huku ikiongozwa na maaskofu Hilikia Omindo (Dayosisi ya Mara) pamoja na John Adiema (kutoka Dayosisi ya Rorya) wote kutoka Kanisa la Anglikana.
Wanahabari na waombolezaji anuai juzi jijini Dar es Salaam walishiriki kuuaga mwili Edward Ogunde kabla ya kusafirishwa kuelekea wilayani Serengeti kwa shughuli za maziko.
Umati huo wa waombolezaji ukiongozwa na viongozi kadhaa wa vyama vya siasa na wamiliki wa vyombo vya habari ulikusanyika jijini Dar es Salaa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo ndipo ilipofanyika ibada ya kumuombea marehemu Ogunde kabla ya kutoa heshima zao za mwisho kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
Upande wa wamiliki wa vyombo vya habari uliongozwa na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi huku vyama vya upinzani vikiwakilishwa na Mwenyekiti wa CUF, Taifa Prof. Ibrahim Lipumba na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiwakilishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mengi alisema vifo vya wanahabari vimekuwa vikiwaathiri wamiliki wa vyombo vya habari kwa kiasi kikubwa pamoja na wadau wengine wa tasnia hiyo, hivyo kuwatia moyo waombolezaji kuendelea kumuombea marehemu Willy Ogunde. Kwa upande wake Prof. Lipumba alisema tasnia ya siasa imepoteza mtu muhimu ambaye ndiye mpigania demokrasia kwenye ushindani wa kisiasa.
“Vyombo vya habari ni muhimu katika ushindani wa kisiasa hasa kidemokrasia…kupoteza mwanahabari kwa njia yoyote tunaathirika wanasiasa…lakini njia pekee ya kumuenzi marehemu Willy ni kuendeleza yale yote mema ambayo alikuwa akiyaamini na kuyasimamia,” alisema Prof. Lipumba.
Marehemu alifariki dunia ghafla mjini Morogoro baada ya kuanguka usiku nyumbani kwa ndugu yake, alipokuwa amekwenda kuwasalimu watoto wake ambao huishi hapo. Marehemu Edward alikuwa mjini Morogoro akihudhuria semina ya wanahabari iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini.
‘Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Willy Edward Ogunde,
Siri nzito yaibuka sakata la madereva wa wabunge
SIRI nzito imeibuka sakata la madai ya madereva wa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo imeelezwa kuwa wabunge wanaoogoza kuwatimu madereva wao ni wa vyama vya upinzani ikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao baadhi yao wamekuwa wakijiendesha wenyewe na kushindwa kupeperusha bendera ya bunge.
Inadaiwa mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM) na mbunge Zitto Kabwe ambaye ni Waziri kivuli wa fedha na uchumi (Chadema) wakiibuka kuwatetea madereva hao kuwa wanapaswa kulipwa vizuri kama ambavyo wabunge wenzao wamekuwa wakijitetea kuhusu maslahi mazuri Kwao wafanye hivyo hata kwa kupigania bungeni maslahi mazuri ya madereva wao badala ya kuwapunja haki zao.
Filikunjombe ambaye amekuwa mbunge wa kwanza katika bunge hilo kufunguka kuguswa na malalamiko hayo ya madereva na hata kuwaunga mkono madereva hao kwa kuwataka kuondoa uoga katika kupigania maslahi yao.
Alitoa kauli hiyo jana wakati akizungunza na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na Madai hayo ya madereva na kudai kuwa amesikitishwa sana kuona madereva wakiendelea kupunjwa haki zao wakati kazi wanazozifanya za kuwaendesha wabunge hao ni kubwa zaidi na kuwataka wabunge wenzake kuwa na roho za huruma kwa madereva hao.
Hata hivyo alishauri wabunge wenzake kujaribu kuwatetea madereva wa wabunge ili Kama inawezekana basi madereva hao waweze kulipwa kama madereva wa mawaziri badala ya posho na Mishahara yao kupitia kwenye akaunti za wabunge.
” Mimi ninawsunga mkono madereva na nitaendelea kufanya hivyo hadi watakavyotendewa haki …hoja ya madereva kuhusu ajali za Mara kwa Mara kwa wabunge wanaojiendesha wenyewe ni ya Msingi zaidi na wabunge wenzangu wanapaswa kuifanyia kazi kuacha kufanya kazi ya udereva hata Kama ni dereva”
Kwa upande wake Mbunge Zitto Kabwe alisema kuwa madereva wanapaswa kuendeleza moto huo ambao wameuwasha bila kuchoka na kuwa tabia ya madereva hao wamekuwa wakianzisha suala hilo na kabla ya kufika mwisho wamekuwa wakiliacha hewani.
Zitto alisema kwa safari hii ataungana nao kupigania maslahi yao na kuwataka madereva hao kuendelea kujenga hoja zaidi ili kuweza kutendewa haki bila ya kugombana na wabunge hao ambao ni mabosi wao.
Alisema kuwa kuanzia mwezi ujao kila mbunge atapewa kiasi cha shilingi 170,000 kwa ajili ya kumlipa dereva wake kila mwezi na kuwa ni vema fedha hizo wabunge kuingia mikataba na madereva hao na mikataba hiyo Kusainiwa na katibu wa bunge ili iwe ya kisheria na fedha hizo kuingizwa moja kwa moja katika akaunti zao.
Zitto alithibitisha Madai ya madereva hao kuwa ni kweli Kabisa wabunge wengi katika bunge hilo hawana madereva na wamekuwa wakila fedha ndogo ambavyo zimekuwa zikitolewa na bunge kwa ajili ya madereva.
Alisema kuwa kwa kuwa mbunge amekuwa akilipwa kiasi cha shilingi 80,000 kwa siku kwa ajili ya posho ni vema kuwepo utaratibu wa kumlipa dereva wake nusu ya fedha hizo kwa kazi anayoifanya badala ya wabunge kuwalipa shilingi 20000 ama chini ya hapo
Zitto alisema kuwa kazi ya madereva ni kubwa hivyo wabunge wanapaswa kuacha mchezo katika kutambua kazi ya madereva hao na kuachana na ubaili usio na maana katika kuwalipa haki stahiki .
“…nasema nitasimama kidete kutetea haki za madereva ili kuona nao wanatendewa haki…suala hilo la madereva kulalamika juu ya maslahi duni kwa mara ya kwanza lilipoibuka zaidi ya miaka miwili sasa mimi niliungana nao kuwatetea na sasa nitaendelea kufanya hivyo,”
Kuhusu Madai ya wabunge wengi wa Chadema kuongoza kutimua madereva na kujiendesha wenyewe na baadhi ya wabunge wa viti maalum kuendeshwa na waume zao, Zitto alitaka wabunge hao pia kuhojiwa wenyewe badala ya kuwasemea yeye. Mbali ya wabunge wa majimbo kujiendesha kwa upande wa wabunge wa viti maalum wamekuwa wakiendeshwa na waume zao huku baadhi yao wakilala kitanda kimoja zaidi ya watatu imefahamika.
Mmoja Kati ya wabunge wa viti maalum wa vyama vya upinzani amedokeza Siri nzito hiyo kwa wabunge na kudai kuwa wabunge hao wamekuwa wakifanya hivyo kwa kuishi maisha ya gheto wawapo bungeni Kama njia ya kubana matumizi .
Pia alisema kuwa mbali ya wabunge kushindwa kuwalipa vizuri madereva wao pia sehemu kubwa ya wabunge wameamua kuegesha mashangigi ya ubunge ambayo walikopeshwa na kutumia magari ya hari ya chini zaidi kutokana na mashangingi hayo kuonekana kutumia mafuta mengi zaidi.
Kwani wamedai kuwa njia hiyo itawasaidia zaidi kujua umma kujua jinsi ambavyo wabunge hao wanavyoongoza kuwatetea wanyonge wakati wao wakiendelea kuwatendea ndivyo sivyo madereva wao.
Madereva hao wamesema kuwa wabunge wamekuwa mbele kutetea madereva wanaofanya kazi hiyo hapa nchini kupewa mikataba wakati kwa upande wao wabunge hao wamekuwa wakiendelea kuwafanyia ufisadi kwa kutowalipa fedha zao wala kuingia mikataba ya kisheria.
Uamuzi huo wa madereva hao kutaka kuwaanika katika vyombo vya habari wabunge hao umetolewa leo tena ikiwa ni siku mbili baada ya blog ya Francis Godwin kuandika juu ya madai ya madereva hao kwa mabosi wao ambao ni wabunge.
Mwenyekiti wa chama cha madereva wa wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Juvenille Joseph alisema kuwa wapo baadhi ya wabunge wachache wa CCM na wale wa vyama vya upinani ambao wamekuwa wakiongoza kwa kuwajali madereva wao .
Ila alisema wapo baadhi ya wabunge ambao madereva wao hata kulala kwao na kula kwao wakiwa bungeni Dodoma ni shida na kuwa baadhi ya madereva wanaolipwa vizuri wamekuwa wakiwachangia fedha za kununua mihogo na maji .
Hivyo alisema kuwa uwazi wa madereva hao kwa kuanika majina ya wabunge wao ambao wamekuwa wakiwapunja haki zao itasaidia kupata haki yao badala ya kuendelea kuwa madereva wa majina na heshima wakati mfukoni hawana kitu.
“Mbali ya wabunge kufanya kazi nao bila mikataba ila baadhi ya wabunge wamekuwa wakilipa vizuri akiwemo bosi wangu Felista Bulla (CCM) mimi kiukweli analipa vizuri sana tofauti na wenzangu ila bado nitaendelea kupigania haki ya madereva wenzangu…,mimi wakati bunge la mwaka 2005 alinipa milioni 3,”
Wabunge wengine waliotoa mkono wa ahsante kwa madereva wao ni pamoja na mbunge, Stella Manyanya (CCM) milioni 5.5, Zitto Kabwe (Chadema) milioni 5.5 na mbunge mmoja wa viti maalum kutoka Zanzibar yeye alimpa dereva wake milioni 3 japo hakurudi bungeni.
“Wabunge wetu wanaongoza kwa kuikosesha serikali mapato yake na ajira kwa vijana kupungua kutokana na baadhi yao kushindwa kutoa mikataba ya kazi wala kuwalipa mishahara ambayo serikali kupitia bunge ilipendekeza kwa ajili ya madereva wa wabunge toka mwaka 2008.”
Hata hivyo alimpongeza mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) kuwa ameonekana kuwa mbunge aliyeingia bungeni kwa kipindi hiki cha kwanza na kuwa mfano wa kumjali dereva wake.
Madereva hao walisema kuwa sehemu kubwa ya wabunge hao wameanza kuendesha magari yao wao wenyewe baada ya kushindana na madereva waliokuwa wakiwaendesha awali baada ya kushindwa kuwalipa mishahara na posho zilizobainishwa kisheria na ofisi ya bunge.
Hata hivyo walisema kuwa suala hilo la wabunge kushindwa kuwalipa vizuri madereva si kwa wabunge wa CCM pekee bali ni wabunge karibu wote wakiwemo wa vyama vya upinzani ambao baadhi yao kwa sasa wanajiendesha wenyewe baada ya kukimbiwa na madereva wao kwa kushindwa kuwalipa.
Pia walisema matukio ya ajali kwa wabunge yamezidi kuongezeka kutokana na wabunge hao kushindwa kufanya kazi na madeva na kuishia kuifanya kazi hiyo wao wenyewe na matokeo yake kutokana na mawazo ama kuwa na mambo mengi kichwani wamekuwa wakishindwa kuyamundu magari yao na kuishia kusababisha ajali za barabarani ambazo baadhi ya ajali hizo zimekuwa zikisababisha vifo ama ulemavu kwa wabunge hao.
“Leo ukitazama hapa bungeni Dodoma utaona idadi kubwa ya wabunge wanajiendesha wenyewe kama si mbunge kuwaendesha wenzake basi mbunge amekuwa akijiendesha mwenyewe na wapo wanaokuja na madereva hadi hapa Dodoma na baada ya hapo dereva amekuwa akipewa nauli ya kurudi jimboni na mbunge anaendelea kujiendesha mwenyewe kama njia ya kubana matumizi,”
Aidha walisema kuwa miongoni mwa madereva waliokosa ajira ni pamoja na wale waliokuwa madereva wa mawaziri na manaibu mawaziri ambao hawakurejea tena baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza mabadiliko ya baraza la mawaziri hivi karibuni ambapo mawaziri hao kwa sasa wamegeuka kuwa madereva wenyewe.
Makamu mwenyekiti wa chama cha madereva wa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Adam Said alisema kuwa sababu ya wabunge wengi kukimbiwa na madereva ni kutokana na maslahi duni wanayoendelea kulipwa na kuwa hivi sasa baadhi ya wabunge baada ya kukimbiwa na madereva wamelazimika kuwatumia ndugu zao kama njia ya kukwepa kuwalipa mishahara .
Pia alisema maisha ambayo madereva hao wamekuwa wakiishi mjini Dodoma ni heri ya omba omba kutokana na wabunge hao kuwalipa kiasi cha shilingi 50,000 ama chini ya hapo na kutaka kuitumia kwa muda wa wiki moja ama mwezi mzima jambo lililopelekea madereva hao kupanga vyumba mtaani na kuishi katika chumba kimoja zaidi ya watatu kama sehemu ya kubana matumizi.
Mwenyekiti wa chama cha madereva wa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Juvenille Joseph alithibitisha madaia ya madereva hao na kuwa tayari uongozi wake umefikisha malalamiko ya madereva hao katika ofisi ya chama cha wafanyakazi mkoa wa Dodoma pamoja na ofisi ya spika wa bunge Anne Makinda ili kushughulikia madai hayo.
Alisema kuwa kwa sasa wanakusudia kuitisha mkutano wa dharura wa madereva wote wanaowaendesha wabunge ili kuweza kuwa na msimamo wa pamoja katika kupigania haki zao na baada ya hao watawatumia barua wabunge ambao wanajiendesha wenyewe ili waweze kujiunga na chama hicho cha madereva wa wabunge .
Kwani alisema kuwa katika barua iliyotolewa na ofisi ya bunge Novemba 3 mwaka 2008 barua yenye kumbukumbu namba FA.155/206/01/70 ikiwa na kichwa yahusu posho ya ubunge Malimbikizo July–Octoba 2008 ilibainisha posho na mishahara hiyo.
Joseph alisema kuwa posho ya mafuta lita 1000 kwa lita shs 2500 kwa wakati huo ilikuwa ni kiasi cha shs milioni 2.5 kwa mwezi, Matengenezo yagari asilimia 40 ya thamani ya mafuta ambayo ilikuwa ni milioni 1 kwa mwezi, posho ya dereva siku 10 kwa shilingi 30,000 (vijijini ) ilikuwa ni shilingi 300,000 na posho ya mbunge siku 10 kwa kila atakazokuwepo kijijini kwa kila siku shs 45,000 ilikuwa ni shs 450,000 huku mshahara wa dereva kwa mwezi ulikuwa ni shs 100,000 na kufanya jumla kwa mwezi kuwa bajeti ya shs milioni 5,115,000 kwa wakati huo.
Ila pamoja na sasa posho za wabunge kupanga ila bado wabunge wamekuwa wakiwalipa madereva wao kiasi cha shs 70,000 hadi 90,000 kwa mwezi fedha ambazo haitoshi kwa maisha ya sasa hivyo kutaka fedha za madereva kuingizwa katika akaunti zao na madereva wote wa wabunge kuwa na mikataba ya kazi badala ya kuendelea kufanya kazi kirafiki na kindugu.
Gap: Let burn churches hooligans Zanzibar

Kardinal Polykarp glorious Gap
Yamola Ibrahim
Head of State Supreme Bishop of Dar es Salaam, Cardinal Polycarp glorious gap has urged the Government of Zanzibar (SMZ), 'control hooligans who want to disrupt peace islands'.
A statement that the gap is the first since the emergence of violence in Zanzibar earlier this month, causing damage to property, while churches yakilengwa more and group kinachojiita of Community Revival and Lectures Islamic (JUMIKI). Gap gave a statement during the service specializing held in the Church of the Cross Bagamoyo in Coast Region, including the preparation of the General Assembly of the Organization of the Holy Spirit, to be held for 30 days from yesterday. Cardinal Gap said, 'hooligans unable to Subdue Competitive Government attention'. "our churches yamecomwa fire and criminals. If the government is and can not take action against criminals, security where are you "he asked Cardinal Gap. "thugs can kutuunguzia seven churches to beat, but before that there are several churches that yalikwishaunguzwa and demolished by the hooligans," he sema.Pengo continued questioning , "If now hooligans have triumphed over strong government of the people that we will be devoured by hooligans and do what they want, we wonder we go? Immediately after the violence in Zanzibar, a panel of bishops from different denominations, they held talks with the Revolutionary Government of Zanzibar (SMZ), while they accuse failing to control the actions of fire burning churches and kuihadharisha take action quickly. Yesterday, Gap he asks the agency to help Bishop Augustine Catholic Diocese of Zanzibar Shayo, harness their energy in the process of consolidating peace.
Gap said apart from such violence, now slavery still continued conditions get in, especially for leaders of government oppressing the people of the lower. He said there are some leaders who want slavery continue to exist for their actions against citizens. "Tanzania is a free equivalent, but I do not believe that it is free for everyone and every Tanzanian, there are people who would like them to waneemeke even with the effects of many without mercy until this day, "he said, adding: "From the School of St. Marian inaanzishwa, there are some leaders have been wanting their children and read it there and the poor children from getting a foothold. " Alitoboa secret that 'there is a letter of application non-core which has been sent Bishop Shayo and declined, and sometimes has been threatened with life, because there are those who want manage the children in good schools to vie kujineemesha. Now this is not slavery? '
Cardinal Gap was called on the Organisation of the Holy Spirit to use the conference to continue promoting peace in the country and glance Zanzibar, where peace inavurugika for the actions of people he called criminals. Conference Organization According to the deputy head of the Holy Spirit, Fr John Kuff from Ghana, conference takes place Africa for the first time since the establishment of the agency in 1868. Tanzania is hosting the meeting of 20 who has been held every after six years, and a final meeting was held in Portugal in 2004. Some countries zitakazoshiriki meeting is Canada, Nageria, Portugal, France, Ghana, England, Irand and host Tanzania. " Referring agency, Gap said while starting to work in, they found peace imevurugika, but they do great work peace ikarejea, so he had wanted to manage the truth even if other people will be cynical. physician pledges peace Delivering greetings of the Government to church there, the District of Bagamoyo, Ahmed physician said conference participants to be at peace because the protection will be strengthened at all. "For all day the 30th of this meeting defense and security will be strengthened to ensure you reach your goals," said the physician.
Ripoti ya gazeti la Nipashe kutoka mikoani kuhusu mgomo wa Madaktari
Mgomo ulioitishwa na madaktari nchi nzima kuanzia jana, umeonekana kutekelezwa katika baadhi ya hospitali nchini huku zingine madaktari wakiendelea na kazi kama kawaida.
Hospitali ambako mgomo huo umeonekana dhahiri ni hospitali za mkoa wa Mwanza, Mbeya na Kilimanjaro na hali imeonekana shwari katika mikoa ya Singida, Dodoma, Arusha, Tanga na Dar es Salaam ukiacha hospitali ya Muhimbili ambako ulionekana mgomo wa chini chini.
Uchunguzi unaonyesha kuwa wale walioendelea na kazi wanadai kuwa hawaoni sababu ya mgomo lakini wanajikuta wakiburuzwa na madaktari wakubwa.
Kwa upande wa Dar es Salaam, mgomo huo umeonekana kuwaathiri wagonjwa wanaopata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, lakini wale wanaotibiwa hospitali za Temeke, Ilala na Mwananyamala, wanaendelea kuhudumiwa na madaktari wao.
Kutokana na hali hiyo, askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), walionekana kuhamisha wagonjwa wao kutoka wodi ya Kibasila katika hospitalini ya Muhimbili na kuondoka nao. Hata hivyo, kitengo cha dharura kilionekana kupokea wagonjwa kama kawaida.
Timu ya waandishi wa NIPASHE Jumapili iliyofika katika hospitali mbalimbali jijini Dar es Salaam ilikwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili na kushuhudia huduma kudorora na baadhi ya wagonjwa wakilalamika kutoonana na madaktari licha ya kupewa ahadi ya kuonana nao.
“Tulisikia madaktari watagoma, inawezekana tayari wameanza mgomo huo, kwani tangu asubuhi mgonjwa wangu hajatembelewa na daktari yeyote zaidi ya kushughulikiwa na wauguzi,” alisema mmoja wagonjwa waliokuwepo hospitalini hapo.
Hata katika kitengo cha mapokezi, ilishuhudiwa hakuna mhudumu yeyote wa hospitali hiyo wala mgonjwa aliyetakiwa kuhudumiwa, licha ya mmoja wafanyakazi hospitalini hapo kuulizwa, na kusema huduma kwa leo (jana) hakuna.
Wakati mgomo huo ukionekana kuanza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kitengo cha dharura kilionekana kuendelea na kazi kama kawaida.
“Kitengo cha dharura kimepewa kuendelea kufanya kazi kwa leo tu (jana), lakini kesho (leo), shughuli zote zitasimama,” alisema daktari mmoja aliyeomba kutotajwa jina lake.
Lakini wakati mgomo huo ukionekana kuanza kuvuta kasi Muhimbili, hospitali ya Manispaa Temeke, hali ilikuwa tofauti kwani huduma kwa wagonjwa ziliendelea kama kawaida huku madaktari wote wakiwepo kazini.
Akizungumza na gazeti hili, Ally Ramadhani aliyelazwa wodi ya wanaume hospitali ya Temeke, alisema wanashukuru Mungu kwa kuweza kuhudumiwa na madaktari waliopuuzia mgomo huo.
“Kama unavyoona, hapa hakuna mgomo wowote, na madaktari wanaendelea kutuhudumia kama kawaida, hao waliogoma ni wa huko huko kwingine,” alisema Ramadhani.
“Katika mgomo wa awali, tulidhani tutanufaika, lakini walionufaika ni madaktari wakuu (MD), lakini wale wasaidizi na wauguzi, hakuongezea chochote na serikali…sasa kwanini tugome wakati hatuna manufaa nao,” alisema mmoja wa madaktari hao.
Alisema, ingawa hospitali ya Temeke ina madaktari wakuu (MD) nane, lakini wote hao wameungana na wengine kuendelea kufanya kazi bila kishawishi chochote cha kuunga mgomo ulioitishwa na madaktari.
Aidha, madaktari hao wamesema wameamua kuendelea na kazi kutokana na kuepusha na madhara ambayo yanaweza kuipata jamii, wakiwemo wao ambao nao wana ndugu zao wanahitaji kupata huduma ya afya nchini kote.
Katika Hospitali ya Manispaa ya Ilala, kumekuwa na utofauti wa huduma kwa madaktari kutokana na madaktari (MD) kuitikia wito wa mgomo, huku wasaidizi (AMO) na wauguzi wakiendelea na kazi kama kawaida, hali iliyofanya wagonjwa kuendelea kupewa huduma wanazostahili.
Aidha, hospitali ya Mwananyamala iliungana na hospitali nyingine za jijini la Dar es Salaam, kuendelea kutoa huduma kama ilivyo kwa Temeke na Ilala.
KCMC WAANZA MGOMO
Madaktari katika hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi, wameanza mgomo rasmi ikiwa ni njia ya kuishinikiza serikali kukamilisha madai yao wanayosema ni ya msingi.
NIPASHE Jumapili, ilifika hospitalini humo na kubaini kuwa baadhi ya madaktari wanaendelea na kazi huku wengione walishaweka zana chini tangu ilipofika majira ya saa 6 usiku na kwamba mgomo huo utapamba moto Jumatatu siku ambayo ina wagonjwa wa nje lakini kwa siku za mwisho wa wiki madaktari wengi wapo mapumziko.
Wakizungumza na NIPASHE Jumapili, baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamelazwa hospitalini humo katika wodi ya watoto walisema kuwa, jana walitangaziwa kabisa kuwa kuanzia leo (jana) kutakuwa na mgomo hivyo wagonjwa wenye nafuu waliruhusiwa kutoka hospitalini humo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka hospitalini humo, Menejimenti ya hospitali hiyo ilikutana na madaktari bingwa na kuzungumza nao, ili kuwasihi kufanyakazi ambazo zinafanywa na madaktari walio kwenye mgomo ili kuokoa jahazi.
Mmoja wa daktari ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema tangu majira ya saa 6 usiku alishaweka zana chini, na kwamba wachache sana ndio wanaendelea na kazi na wengi wakiwa ni wale ambao imani zao za dini haziwaruhusu kugoma kama watawa, mapadri na wachungaji.
TANGA WAENDELEA NA KAZI
Wakati madaktari wakiendelea na mgomo katika baadhi ya mikoa hapa nchini, hali imekuwa tofauti katika hospitali za mkoa wa Tanga ambapo madaktari wameonekana wakiwepo kwenye vituo vyao vya kazi kama kawaida na kusababisha ugumu wa kubashiri iwapo wapo kwenye mgomo au la.
Katika uchunguzi wa gazeti baadhi ya madaktari wameonekana kutokuwa na maamuzi ya nini cha kufanya kutokana na madai ya kutopokea taarifa yoyote ya mgomo katika vyombo vinavyotambulika kisheria .
“Hatuwezi kusema tumegoma au hatukugoma kwa sababu mpaka sasa hakuna mwelekeo wowote na leo ni week end wengi wapo majumbani lakini mpaka Jumatatu tutakuwa na msimamo wa pamoja kimsingi hizi ni haki zetu na lazima tujitetee,“ alisema mmoja wa madaktari katika moja ya hospitali za mkoani hapa kwa sharti la kutotajwa jina lake.
Hata hivyo akizungumzia hali hiyo Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) mkoa wa Tanga, Jacob Barnabas, alisema kuwa mpaka sasa hajapokea taarifa zozote za kuwepo kwa mgomo wa madaktri katika hospitali za mkoa huo.
“Nimekuwa nikiwasiliana na wenyeviti wangu wa matawi lakini hakuna hata mmoja aliyenipa taarifa za kuwepo kwa mgomo sasa ngoja tuone mpaka jumatatu hali itakuaje lakini leo wanaendelea na kazi kama kawaida”,alisema Barnabas.
Alisema kuwa ofisi ya TUGHE Mkoa haijapokea barua yoyote kutoka makao makuu inahusiana kutakiwa kufanya mgomo wa watumishi hao.
MBEYA
Katika Hospitali ya Rufaa Mbeya ofisi za madaktari zilikuwa zimefungwa jana asubuhi na kusababisha msongamano wa wagonjwa katika eneo la mapokezi ya hospitali hiyo, ambako wauguzi waliokuwa zamu walikuwa wakiwaandikisha wagonjwa lakini wakishindwa kuwapa maelekezo ya wapi waende kupata huduma.
Nje ya hospitali hiyo na ile ya wazazi iliyopo eneo la Meta mjini hapa, NIPASHE Jumapili lilishuhudia kukiwa kumebandikwa matangazo ambayo yalionyesha kuwa hapatakuwepo na huduma kutokana na kuanza kwa mgomo wa madaktari.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk. Eliuter Samky, alisema kuwa madaktari walioingia kazini jana walikuwa ni 10 tu kati ya madaktari 80 waliopo hospitalini hapo.
Hata hivyo, Dkt. Samky alisema kuwa ana uhakika kwamba idadi ya madaktari watakaoendelea na kazi itaongezeka Jumatatu kwa vile jana ilikuwa ni siku ya mapumziko.
Baadhi ya akina mama waliolazwa na watoto wao katika Hospitali ya Rufaa Mbeya wameitaka Serikali kuharakisha kushughulikia tatizo hilo ili kuepusha vifo vinavyoweza kutokea kutokana na wagonjwa kukosa huduma za madaktari waliogoma.
Kwa mujibu wa matangazo yaliyobandikwa kwenye mbao za matangazo na kwenye kuta nje na ndani ya hospitali ya Rufaa Mbeya na ile ya Wazazi Meta, mgomo huo umeanza baada ya majadiliano kati ya serikali na kamati ya madaktari kushindwa kufikia muafaka, hivyo kamati maalum ya madaktari imeamua kutangaza mgomo usiokuwa na kikomo kwa kusitisha utoaji wa huduma kuanzia jana, Juni 23, 2012.
Taarifa hiyo pia iliwataka wananchi wenye matatizo ya kiafya wakatafute huduma sehemu nyingine ili waweze kupata huduma.
Baada ya kutembelea wodi ya watoto nambari 5 na 6 mwandishi wa habari hii alishuhudia wazazi wa watoto wakiwa wamekaa vikundi wakiwa na nyuso za huzuni huku wakionyesha hofu ya watoto wao kupata matibabu kutokana na mgomo huo.
Baadhi ya wauguzi waliokuwa katika mawodi na kuendelea kuhudumia wagonjwa walilazwa hospitali, walikataa kuzungumzia hali ya wagonjwa kukosa huduma za madaktari kwa madai kuwa wao sio wasemaji, ingawa walilalamika kuwa kutokuwepo kwa madaktari kazini kunasababisha na wao washindwe kufanya kazi zao kwa ufasaha.
MWANZA
Madaktari zaidi ya 200 waliopo katika Hosptali ya Rugfaa ya Bugando jijini Mwanza jana wameanza mgomo rasmi baada ya serikali kushindwa kutoa majibu ya kuridhisha kuhusu madai yao mbalimbali yaliyosababisha madaktari hao kugoma mapema mwaka huu.
Akizungumza na NIPASHE Jumapili jijini hapa jana, mwakilishi wa kamati ya kufuatilia madai ya madaktari hao, Dkt. Richard Kirita alisema kwamba madaktari wa kada zote katika hospitali hiyo wapo kwenye mgomo isipokuwa baadhi ya Madaktari Bingwa pamoja na Wakuu wa Idara.
Hata hivyo, alisema kwamba wanaendelea na vikao ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na wenzao wa Dar es Salaam ili kujua ni hatua zipi zaidi wachukue kuhusiana na mgomo wao huo.
Alisema kwamba katika kikao cha madaktari wa Bugando kilichofanyika hivi karibuni kilihusisha jumla ya madaktari 202 kwa ajili ya kujadili hatma ya madai yao kwa serikali ambapo walikubaliana kwa pamoja kuanza mgomo ifikapo Juni 23 (jana) iwapo madai yao yangekuwa hajatekelezwa na serikali.
Baadhi ya watu waliokuwa wamepeleka wagonjwa katika hospitali hiyo jana walionekana wakiwaondoa baada ya kukosa huduma kutoka kwa madaktari ambao baadhi walikuwa kwenye kikao na wengine walionekana katika vikundi vikundi wakipiga soga.
ARUSHA
Hali ya huduma katika hospitali ya Mount Meru katika Mkoa wa Arusha ni shwari, licha ya madaktari kutangaza mgomo nchi nzima.
NIPASHE ilishuhudia wagonjwa wakipata huduma stahili katika hospitali hiyo na zahanati zake za Kaloleni na Levolosi bila kuwepo kwa manung'uniko yoyote toka kwa wagonjwa.
Akizungumza na NIPASHE mmoja wa wagonjwa katika hospitali ya Mkoa ya Mounti Meru, John Samweli, alisema kuwa alifika katika hospitali hiyo asubuhi jana na amepokelewa vizuri na kupatiwa huduma bila kupata shida.
John aliomba serikali kutfakari kwa makini na kucha kutoa majibu mepesi kwa madaktari hao wanaodai stahiki zao, ambazo walikubalina na serikali na hawajapata.
Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Eliringia Mlay akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu ya kiganjni, alijibu kwa ufupi kuwa mgomo haupo.
SINGIDA
Huduma za tiba katika hospitali ya mkoa wa Singida na za Wilaya ya Manyoni, Iramba na Halmashauri ya wilaya ya Singida zimeendelea kama kawaida kinyume na ilivyotangazwa kwamba kutakuwa na mgomo wa madaktari nchi nzima.
NIPASHE ilifika katika hospitali hizo na kushuhudia shuguhuli za huduma za afya zikiendelea kama kawaida huku wauguzi na madaktari wakiwa katika nyuso za furaha wakidai kuwa mgomo huo hauwahusu labda wenzao wa jijini Dar es Salaam na mikoa mingine mikubwa.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi katika hospitali ya Singida, Dk. Joseph Malunda, alisema kimsingi hakuna mgomo wowote na shughuli za tiba zinaendelea kama kawaida.
Mmoja wa wagonjwa aliyejitambulisha kwa jina la Fatma Mitigo alisema tangu alipofika hospitalini hapo amepatiwa matibabu kwa wakati.
DODOMA
Licha ya madaktari mkoani Dodoma kutoa msimamo wa kuunga mkono mgomo wa kitaifa wa madaktari, huduma za matibabu katika hospitali ya mkoa zimeendelea kama kawaida.
Uchunguzi wa NIPASHE Jumapili uliohusu mahojiano na baadhi ya wagonjwa mawodini na Mganga Mkuu wa Hospitali Dk. Ezekiel Mpuya, ulibaini kuwa hakukuwa na mgomo jana.
Baadhi ya wagonjwa wa wodi namba 16-A wanaosumbuliwa na shinikizo la damu na kisukari walieleza kuwa walionwa na matabibu, walipata dawa na wauguzi wa zamu wamekuwa wakiwahudumia.
Katika wodi ya watoto pamoja na ya wazazi hali ilikuwa shwari , shughuli ziliendelea kama kawaida. Kwa upande wake Mganga Mkuu, alisema hakuna aliyegoma na huduma zinaendelea kutolewa.
Source: http://www.wavuti.com
Hospitali ambako mgomo huo umeonekana dhahiri ni hospitali za mkoa wa Mwanza, Mbeya na Kilimanjaro na hali imeonekana shwari katika mikoa ya Singida, Dodoma, Arusha, Tanga na Dar es Salaam ukiacha hospitali ya Muhimbili ambako ulionekana mgomo wa chini chini.
Uchunguzi unaonyesha kuwa wale walioendelea na kazi wanadai kuwa hawaoni sababu ya mgomo lakini wanajikuta wakiburuzwa na madaktari wakubwa.
Kwa upande wa Dar es Salaam, mgomo huo umeonekana kuwaathiri wagonjwa wanaopata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, lakini wale wanaotibiwa hospitali za Temeke, Ilala na Mwananyamala, wanaendelea kuhudumiwa na madaktari wao.
Kutokana na hali hiyo, askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), walionekana kuhamisha wagonjwa wao kutoka wodi ya Kibasila katika hospitalini ya Muhimbili na kuondoka nao. Hata hivyo, kitengo cha dharura kilionekana kupokea wagonjwa kama kawaida.
Timu ya waandishi wa NIPASHE Jumapili iliyofika katika hospitali mbalimbali jijini Dar es Salaam ilikwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili na kushuhudia huduma kudorora na baadhi ya wagonjwa wakilalamika kutoonana na madaktari licha ya kupewa ahadi ya kuonana nao.
“Tulisikia madaktari watagoma, inawezekana tayari wameanza mgomo huo, kwani tangu asubuhi mgonjwa wangu hajatembelewa na daktari yeyote zaidi ya kushughulikiwa na wauguzi,” alisema mmoja wagonjwa waliokuwepo hospitalini hapo.
Hata katika kitengo cha mapokezi, ilishuhudiwa hakuna mhudumu yeyote wa hospitali hiyo wala mgonjwa aliyetakiwa kuhudumiwa, licha ya mmoja wafanyakazi hospitalini hapo kuulizwa, na kusema huduma kwa leo (jana) hakuna.
Wakati mgomo huo ukionekana kuanza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kitengo cha dharura kilionekana kuendelea na kazi kama kawaida.
“Kitengo cha dharura kimepewa kuendelea kufanya kazi kwa leo tu (jana), lakini kesho (leo), shughuli zote zitasimama,” alisema daktari mmoja aliyeomba kutotajwa jina lake.
Lakini wakati mgomo huo ukionekana kuanza kuvuta kasi Muhimbili, hospitali ya Manispaa Temeke, hali ilikuwa tofauti kwani huduma kwa wagonjwa ziliendelea kama kawaida huku madaktari wote wakiwepo kazini.
Akizungumza na gazeti hili, Ally Ramadhani aliyelazwa wodi ya wanaume hospitali ya Temeke, alisema wanashukuru Mungu kwa kuweza kuhudumiwa na madaktari waliopuuzia mgomo huo.
“Kama unavyoona, hapa hakuna mgomo wowote, na madaktari wanaendelea kutuhudumia kama kawaida, hao waliogoma ni wa huko huko kwingine,” alisema Ramadhani.
“Katika mgomo wa awali, tulidhani tutanufaika, lakini walionufaika ni madaktari wakuu (MD), lakini wale wasaidizi na wauguzi, hakuongezea chochote na serikali…sasa kwanini tugome wakati hatuna manufaa nao,” alisema mmoja wa madaktari hao.
Alisema, ingawa hospitali ya Temeke ina madaktari wakuu (MD) nane, lakini wote hao wameungana na wengine kuendelea kufanya kazi bila kishawishi chochote cha kuunga mgomo ulioitishwa na madaktari.
Aidha, madaktari hao wamesema wameamua kuendelea na kazi kutokana na kuepusha na madhara ambayo yanaweza kuipata jamii, wakiwemo wao ambao nao wana ndugu zao wanahitaji kupata huduma ya afya nchini kote.
Katika Hospitali ya Manispaa ya Ilala, kumekuwa na utofauti wa huduma kwa madaktari kutokana na madaktari (MD) kuitikia wito wa mgomo, huku wasaidizi (AMO) na wauguzi wakiendelea na kazi kama kawaida, hali iliyofanya wagonjwa kuendelea kupewa huduma wanazostahili.
Aidha, hospitali ya Mwananyamala iliungana na hospitali nyingine za jijini la Dar es Salaam, kuendelea kutoa huduma kama ilivyo kwa Temeke na Ilala.
KCMC WAANZA MGOMO
Madaktari katika hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi, wameanza mgomo rasmi ikiwa ni njia ya kuishinikiza serikali kukamilisha madai yao wanayosema ni ya msingi.
NIPASHE Jumapili, ilifika hospitalini humo na kubaini kuwa baadhi ya madaktari wanaendelea na kazi huku wengione walishaweka zana chini tangu ilipofika majira ya saa 6 usiku na kwamba mgomo huo utapamba moto Jumatatu siku ambayo ina wagonjwa wa nje lakini kwa siku za mwisho wa wiki madaktari wengi wapo mapumziko.
Wakizungumza na NIPASHE Jumapili, baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamelazwa hospitalini humo katika wodi ya watoto walisema kuwa, jana walitangaziwa kabisa kuwa kuanzia leo (jana) kutakuwa na mgomo hivyo wagonjwa wenye nafuu waliruhusiwa kutoka hospitalini humo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka hospitalini humo, Menejimenti ya hospitali hiyo ilikutana na madaktari bingwa na kuzungumza nao, ili kuwasihi kufanyakazi ambazo zinafanywa na madaktari walio kwenye mgomo ili kuokoa jahazi.
Mmoja wa daktari ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema tangu majira ya saa 6 usiku alishaweka zana chini, na kwamba wachache sana ndio wanaendelea na kazi na wengi wakiwa ni wale ambao imani zao za dini haziwaruhusu kugoma kama watawa, mapadri na wachungaji.
TANGA WAENDELEA NA KAZI
Wakati madaktari wakiendelea na mgomo katika baadhi ya mikoa hapa nchini, hali imekuwa tofauti katika hospitali za mkoa wa Tanga ambapo madaktari wameonekana wakiwepo kwenye vituo vyao vya kazi kama kawaida na kusababisha ugumu wa kubashiri iwapo wapo kwenye mgomo au la.
Katika uchunguzi wa gazeti baadhi ya madaktari wameonekana kutokuwa na maamuzi ya nini cha kufanya kutokana na madai ya kutopokea taarifa yoyote ya mgomo katika vyombo vinavyotambulika kisheria .
“Hatuwezi kusema tumegoma au hatukugoma kwa sababu mpaka sasa hakuna mwelekeo wowote na leo ni week end wengi wapo majumbani lakini mpaka Jumatatu tutakuwa na msimamo wa pamoja kimsingi hizi ni haki zetu na lazima tujitetee,“ alisema mmoja wa madaktari katika moja ya hospitali za mkoani hapa kwa sharti la kutotajwa jina lake.
Hata hivyo akizungumzia hali hiyo Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) mkoa wa Tanga, Jacob Barnabas, alisema kuwa mpaka sasa hajapokea taarifa zozote za kuwepo kwa mgomo wa madaktri katika hospitali za mkoa huo.
“Nimekuwa nikiwasiliana na wenyeviti wangu wa matawi lakini hakuna hata mmoja aliyenipa taarifa za kuwepo kwa mgomo sasa ngoja tuone mpaka jumatatu hali itakuaje lakini leo wanaendelea na kazi kama kawaida”,alisema Barnabas.
Alisema kuwa ofisi ya TUGHE Mkoa haijapokea barua yoyote kutoka makao makuu inahusiana kutakiwa kufanya mgomo wa watumishi hao.
MBEYA
Katika Hospitali ya Rufaa Mbeya ofisi za madaktari zilikuwa zimefungwa jana asubuhi na kusababisha msongamano wa wagonjwa katika eneo la mapokezi ya hospitali hiyo, ambako wauguzi waliokuwa zamu walikuwa wakiwaandikisha wagonjwa lakini wakishindwa kuwapa maelekezo ya wapi waende kupata huduma.
Nje ya hospitali hiyo na ile ya wazazi iliyopo eneo la Meta mjini hapa, NIPASHE Jumapili lilishuhudia kukiwa kumebandikwa matangazo ambayo yalionyesha kuwa hapatakuwepo na huduma kutokana na kuanza kwa mgomo wa madaktari.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk. Eliuter Samky, alisema kuwa madaktari walioingia kazini jana walikuwa ni 10 tu kati ya madaktari 80 waliopo hospitalini hapo.
Hata hivyo, Dkt. Samky alisema kuwa ana uhakika kwamba idadi ya madaktari watakaoendelea na kazi itaongezeka Jumatatu kwa vile jana ilikuwa ni siku ya mapumziko.
Baadhi ya akina mama waliolazwa na watoto wao katika Hospitali ya Rufaa Mbeya wameitaka Serikali kuharakisha kushughulikia tatizo hilo ili kuepusha vifo vinavyoweza kutokea kutokana na wagonjwa kukosa huduma za madaktari waliogoma.
Kwa mujibu wa matangazo yaliyobandikwa kwenye mbao za matangazo na kwenye kuta nje na ndani ya hospitali ya Rufaa Mbeya na ile ya Wazazi Meta, mgomo huo umeanza baada ya majadiliano kati ya serikali na kamati ya madaktari kushindwa kufikia muafaka, hivyo kamati maalum ya madaktari imeamua kutangaza mgomo usiokuwa na kikomo kwa kusitisha utoaji wa huduma kuanzia jana, Juni 23, 2012.
Taarifa hiyo pia iliwataka wananchi wenye matatizo ya kiafya wakatafute huduma sehemu nyingine ili waweze kupata huduma.
Baada ya kutembelea wodi ya watoto nambari 5 na 6 mwandishi wa habari hii alishuhudia wazazi wa watoto wakiwa wamekaa vikundi wakiwa na nyuso za huzuni huku wakionyesha hofu ya watoto wao kupata matibabu kutokana na mgomo huo.
Baadhi ya wauguzi waliokuwa katika mawodi na kuendelea kuhudumia wagonjwa walilazwa hospitali, walikataa kuzungumzia hali ya wagonjwa kukosa huduma za madaktari kwa madai kuwa wao sio wasemaji, ingawa walilalamika kuwa kutokuwepo kwa madaktari kazini kunasababisha na wao washindwe kufanya kazi zao kwa ufasaha.
MWANZA
Madaktari zaidi ya 200 waliopo katika Hosptali ya Rugfaa ya Bugando jijini Mwanza jana wameanza mgomo rasmi baada ya serikali kushindwa kutoa majibu ya kuridhisha kuhusu madai yao mbalimbali yaliyosababisha madaktari hao kugoma mapema mwaka huu.
Akizungumza na NIPASHE Jumapili jijini hapa jana, mwakilishi wa kamati ya kufuatilia madai ya madaktari hao, Dkt. Richard Kirita alisema kwamba madaktari wa kada zote katika hospitali hiyo wapo kwenye mgomo isipokuwa baadhi ya Madaktari Bingwa pamoja na Wakuu wa Idara.
Hata hivyo, alisema kwamba wanaendelea na vikao ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na wenzao wa Dar es Salaam ili kujua ni hatua zipi zaidi wachukue kuhusiana na mgomo wao huo.
Alisema kwamba katika kikao cha madaktari wa Bugando kilichofanyika hivi karibuni kilihusisha jumla ya madaktari 202 kwa ajili ya kujadili hatma ya madai yao kwa serikali ambapo walikubaliana kwa pamoja kuanza mgomo ifikapo Juni 23 (jana) iwapo madai yao yangekuwa hajatekelezwa na serikali.
Baadhi ya watu waliokuwa wamepeleka wagonjwa katika hospitali hiyo jana walionekana wakiwaondoa baada ya kukosa huduma kutoka kwa madaktari ambao baadhi walikuwa kwenye kikao na wengine walionekana katika vikundi vikundi wakipiga soga.
ARUSHA
Hali ya huduma katika hospitali ya Mount Meru katika Mkoa wa Arusha ni shwari, licha ya madaktari kutangaza mgomo nchi nzima.
NIPASHE ilishuhudia wagonjwa wakipata huduma stahili katika hospitali hiyo na zahanati zake za Kaloleni na Levolosi bila kuwepo kwa manung'uniko yoyote toka kwa wagonjwa.
Akizungumza na NIPASHE mmoja wa wagonjwa katika hospitali ya Mkoa ya Mounti Meru, John Samweli, alisema kuwa alifika katika hospitali hiyo asubuhi jana na amepokelewa vizuri na kupatiwa huduma bila kupata shida.
John aliomba serikali kutfakari kwa makini na kucha kutoa majibu mepesi kwa madaktari hao wanaodai stahiki zao, ambazo walikubalina na serikali na hawajapata.
Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Eliringia Mlay akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu ya kiganjni, alijibu kwa ufupi kuwa mgomo haupo.
SINGIDA
Huduma za tiba katika hospitali ya mkoa wa Singida na za Wilaya ya Manyoni, Iramba na Halmashauri ya wilaya ya Singida zimeendelea kama kawaida kinyume na ilivyotangazwa kwamba kutakuwa na mgomo wa madaktari nchi nzima.
NIPASHE ilifika katika hospitali hizo na kushuhudia shuguhuli za huduma za afya zikiendelea kama kawaida huku wauguzi na madaktari wakiwa katika nyuso za furaha wakidai kuwa mgomo huo hauwahusu labda wenzao wa jijini Dar es Salaam na mikoa mingine mikubwa.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi katika hospitali ya Singida, Dk. Joseph Malunda, alisema kimsingi hakuna mgomo wowote na shughuli za tiba zinaendelea kama kawaida.
Mmoja wa wagonjwa aliyejitambulisha kwa jina la Fatma Mitigo alisema tangu alipofika hospitalini hapo amepatiwa matibabu kwa wakati.
DODOMA
Licha ya madaktari mkoani Dodoma kutoa msimamo wa kuunga mkono mgomo wa kitaifa wa madaktari, huduma za matibabu katika hospitali ya mkoa zimeendelea kama kawaida.
Uchunguzi wa NIPASHE Jumapili uliohusu mahojiano na baadhi ya wagonjwa mawodini na Mganga Mkuu wa Hospitali Dk. Ezekiel Mpuya, ulibaini kuwa hakukuwa na mgomo jana.
Baadhi ya wagonjwa wa wodi namba 16-A wanaosumbuliwa na shinikizo la damu na kisukari walieleza kuwa walionwa na matabibu, walipata dawa na wauguzi wa zamu wamekuwa wakiwahudumia.
Katika wodi ya watoto pamoja na ya wazazi hali ilikuwa shwari , shughuli ziliendelea kama kawaida. Kwa upande wake Mganga Mkuu, alisema hakuna aliyegoma na huduma zinaendelea kutolewa.
Source: http://www.wavuti.com
Subscribe to:
Posts (Atom)













